Alhamisi, 23 Aprili 2015

Sekta yaMifugo ina nafasi kubwa katika kujenga uchumi imara wa Taifa




Sekta ya Mifugo ina nafasi kubwa katika kujenga uchumi imara wa Taifa, kuongeza kipato kwa Watanzania wanaotegemea mifugo, na kutoa fursa za ajira sanjari na kuhifadhi rasilimali za Taifa.


kwa masilia zadi no:0752-2840777


Yapo mabadiliko chanya katika Sekta ya Mifugo nchini ambayo yameanza kujionyesha,hususan katika uzalishaji na uuzaji wa mifugo na ma zao yake nje ya nchi,utoaji wa huduma na upatikanaji wa  pembejeo  za mifugo na hawa mingoni mwa viongzi wa Bina Foundation Singida. 
 Mkazo wa  Bina Foundation utaendelea kuwekwa katika kugharamia huduma za ufugaji zinazoh itajika kukuza sekta kwa ufanisi. Huduma hizo ni pamoja na miundombinu ya vijijini, utafiti huduma za ugani, uzuiaji magonjwa ya mlipuko na udhibiti wa wadudu waenezao magonjwa ya mifugo.


Aidha, Bw. Piter amiomba  Serikali kuhamasisha wafugaji na wadau wengine kuchangia gharama  za utoaji wa huduma kama vile ujenzi wa malambo na majosho nchini.




(TPFC)Ni  Jukwaa la Jamii ya Wafugaji Tanzania (TPCF), juzi lilizindua rasimu ya sera ya ufugaji wa asili nchini, ili iweze kujadilidiwa na wafugaji na baadaye ipelekwe serikalini, ili kusaidia kuandaliwa sera rasmi ya ufugaji wa asili nchini.

wanafunzi kutoka mkoa Dodoma baada ya kupokea msada kutoka kwa wakurugenzi wa Bina Foundation.


Mratibu wa jukwaa hilo, Joseph Parsambei aliwasilisha rasimu ya sera hiyo juzi katika kongamano la jukwaa la wafugaji, lililofanyika Arusha na kuhudhuriwa na wawakilishi wa wafugaji kutoka mikoa ya wafugaji.

Mganga alifanikisha kumzalisha Ngombe Kwa upasuaji katika sehemu ya ufugaji Ndani ya Bina Foundation.

Nguruwe zipo kwa wingi katika mradi wa Bina Foundation Singida.kwa masilia zadi no:0752-2840777

kwa masilia zadi no:0752-2840777


 Bw. Peter Bina bada ya kukutana na waataalam na hapa anaelezea Homa ya Bonde la Ufa (HBU) (Rift valley fever) ni ugonjwa wa kirusi unaojitokeza kwa dharula ukishambulia  hasa wanyama wanaocheua (ngo'mbe, mbuzi, kondoo), lakini wanyama wengine pia hupata kama punda, ngamia na wanyama pori mfano nyati, nyumbu na swala . Mwanadamu pia hupata ugojwa huu kutoka kwa wanyama walio na ugonjwa huu kwa kula nyama isiyopimwa na kupikwa vizuri au kwa kushika mazao ya wanyama wenye ugonjwa . Ugonjwa unasababishwa na virusi vya homa ya bonde la ufa homa (VHBU) vinavyo sambazwa na mbu aina ya Aedes. HBU huleta madhara makubwa sana kiuchumi na kijamii pale unapotokea na hasa hatua za makusudi za kuzuia kuenea kwake zisipo chukuliwa. Kuwepo kwa wanyama wanao tupa mimba kwa wingi kati ya kondoo, mbuzi, ng'ombe na ngamia na vifo vya wanyama wadondo (watoto wa mbuzi, kondoo, na ndama) kwa karibu asilimia mia moja na uwepo wa dalili zinazofanana na mafua ya ndege ni viashilia tosha vya kuwepo kwa HBU. Historia ya kuwepo kwa mvua nyingi kiasi cha kutengeneza mafuriko pamoja na ongezeko la mbu wanaoeneza ugonjwa huu ni kiashiria cha kuanzia kufanya uchunguzi wa kina ili hatua mahususi ziweze kuchukuliwa.

kuku wa kienyeji wanapatika kwa wingi katika mradi wa Bina Foundation Singida


Lakini miaka mitatu iliyopita ulipiga hodi hapa nchini na kuua watu katika mikoa ambayo Bonde la Ufa linapita hasa maeneo ya Arusha na Manyara, Kanda ya Kaskazini mwa Tanzania.
Ugonjwa wa homa ya bonde la ufa ulioonekana kwa mara ya kwanza Kenya, matukio yake makubwa yameonekana katika nchi nyingi za Bara la Afrika, ikiwa ni pamoja na Misri, Sudan, Somalia, Kenya, Msumbiji, Nigeria, Senegal, Tanzania, Uganda, Zambia, Zimbabwe, Namibia na Afrika Kusini.




 kwa masilia zadi no:0752-2840777



Nchi ya Misri ilikumbwa na ugonjwa huu mwaka 1977 na 1978 ambapo watu wapatao 18,000 waliugua na 598 walikufa. Nchi ambazo taarifa zilitolewa za matukio ya ugonjwa huu nje ya Bara la Afrika ni pamoja na Yemen na Saudi Arabia.
Kwa hapa Tanzania ugonjwa huu ulionekana mwaka 1979 na 1998 katika mikoa ya Mara, Arusha na Kilimanjaro ambapo ng’ombe, mbuzi, kondoo na ngamia waliathirika.

HBU ni ugonjwa unaosababishwa na virusi vijulikanvyo kama virusi vya homa ya bonde la ufa (VHBU) vilivyopo kwenye familia ya virusi ya Bunya (Bunyaviridae). VHBU vimekuepo tangu zamani sana na viligunduliwa kitaalamu kwa mara ya kwanza nchini Kenya mnamo mwaka 1931 katika bonde la ufa (Rift Vlley), kiini cha jina la ugonjwa. Vinasaba vya kirusi hiki ni vya aina ya RNA na ina vipingili vitatu ambavyo husaidia kirusi huyu kutengeneza aina nyingine ya kirusi yuleyule na kumfanya asishambuliwe na kinga ya mwili ya mnyama.



kwa masilia zadi no:0752-2840777

Kwale (pia kware) ni ndege wa jenasi mbalimbali katika familia ya Phasianidae. Spishi nne za Francolinus ambazo zina ngozi kichele yenye rangi kali kooni na pande zote za macho huitwa kereng'ende pia. Rangi ya kwale ni kahawia au kijivu na wana michirizi au madoa. Mara nyingi miguu yao ni myekundu au rangi ya manjano na koo lao ni jekundu, jeupe, jeusi au rangi ya manjano. Hujificha kwa kawaida lakini sauti yao husikika mara kwa mara. Chakula chao ni mbegu, wadudu na nyungunyungu. Hutaga mayai matatu hadi kumi ardhini pengine juu ya manyasi makavu.
Karibu spishi zote zinatokea Afrika lakini spishi tano zinatokea Asia.
Kwale (ndege)kwa masilia zadi no:0752-2840777


 kwa masilia zadi no:0752-2840777




Mayai ni bidhaa hafifu na inayoharibika kwa haraka. Hivyo, ni lazima ishikwe kwa uangalifu na kutunzwa vizuri baada ya kutagwa ili yasivunjike au kuharibika. Watu wengi wanaonunua mayai kutoka dukani watatambua mara moja kuwa mayai hayo yamevunjika au yameoza. Tatizo hili linaweza kutokana na utunzaji na uhifadhi wakati mayai bado yakiwa kwa mfugaji.

Ili kupunguza hasara, ni lazima mfugaji ahakikishe kuwa mayai yanafika sokoni yakiwa bado mapya na salama. Utunzaji sahihi wa mayai huyafanya yaepukane na madhara yanayoweza kutokana na viumbe wadogo wadogo kama vile bakteria, wanyama walao mayai, upotevu wa unyevu, au joto wakati wa uhifadhi na kusafirisha kwenda sokoni, jambo linaloweza kuyafanya yavunjike. Mayai kama ilivyo kwa viumbe hai wengine yanahitaji kupumua. Trei za kuhifadhia mayai ziwekwe kwenye sehemu yenye hewa inayozunguka, hasa hewa ya oxyjeni.

Trei zote za kuhifadhia mayai ni lazima ziwekwe katika hali ya usafi, zisiwe na harufu ili kuepuka kufishwa au kusababisha hali yoyote inayoweza kusababisha uharibifu. Mayai ni lazima pia yakingwe dhidi ya joto kali pamoja na unyevu.



Jinsi ya kutunza vifaranga kwa masilia zadi no:0752-2840777



Mayai yanaweza kuharibika kwa haraka kutokana na joto kali. Labda yahifadhiwe kwenye jotoridi la chini, vinginevyo mfugaji atapoteza idadi kubwa ya mayai kabla hayajafika sokoni. Ni lazima kuhakikisha kuwa mayai yanahifadhiwa sehemu yenye ubaridi, ambayo siyo kavu sana, vinginevyo yatapoteza unyevu kwa haraka endapo yatawekwa sehemu kavu. Hali ya mahali pa kuhifadhia inategemea na siku ambazo mfugaji anahitaji kuhifadhi mayai.

Wafugaji wenye uzoefu wamekuwa na uwezo wa kuhifadhi mayai kwa kipindi cha miezi 6-7 kwa kutumia jokofu. Wafugaji wadogo pia wanaweza kuhifadhi mayai kwa siku kadhaa mpaka watakapopata mayai kwa ajili ya kuhatamiwa. Kamwe usihifadhi mayai unayokusudia kutumia kwa ajili ya kuhatamiwa kwenye jokofu.

Uhifadhi wa mayai kwa ajili ya kuhatamia

Wafugaji wadogo hutumia njia ya kiasili kuhatamisha na kuangua mayai. Hii ni njia ya kutumia kuku au ndege mwingine ambaye hupewa mayai na kuyahatamia hadi kuanguliwa. Kuku wa kienyeji ni wazuri sana wanapotumiwa kwa ajili ya uzalishaji wa vifaranga. Hata hivyo kwa uzalishaji mzuri ni lazima mfugaji ahakikishe kuwa kuku anapewa mayai yenye uwezekano mkubwa wa kuanguliwa.

Mbinu moja wapo ambayo mfugaji anaweza kuitumia kutambua mayai yenye uwezekano mkubwa wa kuanguliwa ni kwa kumulika kwa kutumia mshumaa. Mayai yanaweza kuwekwa kwenye mwanga mkali ambao utakuwezesha kuona ndani ya yai. Kifaa rahisi cha kumulika mayai kinaweza kutengenezwa kutokana na kuweka balbu ndani ya boksi dogo. Unakata tundu dogo kuruhusu mwanga. Hakikisha linakuwa na ukubwa wa kuweza kuruhusu yai kukaa juu yake.

Shika yai kwa kulisimamisha kwa kutumia vidole vyako viwili, kasha liweke kwenye mwanga wa tochi au balbu. Zoezi hili linakupa uhakika kuwa mayai yenye uwezekano wa kuanguliwa ndiyo pekee yanayochaguliwa.

Tengeneza sehemu ya kuhatamia mayai

Mfugaji anaweza kuboresha uzalishaji wa kuku wa kienyeji kwa kuwajengea tabia ya kuhatamia mayai. Kuku wa kienyeji wakiwa wamelishwa vizuri, wanaweza kuhatamia kati ya mayai 10-14 kwenye mzunguko mmoja. Baada ya kuangua, mfugaji amruhusu kuku kukaa na vifaranga walau kwa wiki moja. Baada ya hapo vifaranga wanaweza kutengwa.

Kuku wakiwa bado katika hali ya kuhatamia, anaweza kupewa mayai ya bandia ambayo yanaweza kutengenezwa kutokana na sabuni, huku kuku wengine wakiwa wamehatamia mayai halisi ya kutosha. Mayai bandia yanaweza kuondolewa na kuku kuwekewa mayai halisi aendelee kuhatamia mpaka yatakapoanguliwa.

Kuku wanaohatamia ni lazima wapatiwe chakula na maji ya kutosha. Kuku ambao hawahitajiki kwa ajili ya kuendelea kutotoa, wanyang’anywe vifaranga na kuachiliwa walipo kuku wengine. Ni vizuri kuweka alama kila yai kuonesha ni tarehe gani lilitagwa, hii itamsaidia mfugaji kutokuchanganya mayai ya zamani na mayai mapya. Badala yake, mfugaji anaweza kuwatenga kuku ambao amewaandaa
kwa ajili ya kutotoa na wale ambao ni kwa ajili ya kutaga tu ili asichanganye mayai yake.
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 maoni:

Chapisha Maoni

Item Reviewed: Sekta yaMifugo ina nafasi kubwa katika kujenga uchumi imara wa Taifa Description: Rating: 5 Reviewed By: Unknown
Scroll to Top