Ijumaa, 18 Oktoba 2013



                                   Yanga Kampuni yazua mtafaruku Jangwani

Kaimu Katibu Mkuu wa Yanga, Lawrence Mwalusako, alisema jana Jumatano kuwa wanachama hao watatoa maoni kama wanataka Yanga iwe kampuni au iendelee na mfumo wa sasa wa wanachama.

“Wanachama wa Yanga wanatakiwa kutoa maoni yao kwa kupiga kura za ndio au hapana kwenye sanduku la maoni ambalo litakuwa hapa klabuni,” alisema Mwalusako ambaye Mwanaspoti linajua Mkenya, Patrick Naggi atapewa nafasi yake.

Alisema utaratibu huo utafikia tamati Novemba 10 na kwamba mwanachama atalazimika kupiga kura kwa kadi yake ambayo ameilipia, kwani itamthibitisha kuwa ni mwanachama hai na atatakiwa kupiga kura mara moja.

Hata hivyo, wakati Yanga wameanzisha utaratibu huo, Yanga ni klabu pekee, ambayo imeshasajiliwa na Msajili wa Makampuni tangu Juni 28, 2000. Kampuni hiyo ilisajiliwa na kupewa namba 39551 chini ya Francis Kifukwe na ilifikia hatua ya kuuza hisa zake.

Malinzi alishangaa kusikia mchakato huo umetangazwa na kusema: “Yanga siku nyingi sana ilishakuwa Kampuni na tulifikia hatua ya kuuza hisa zake, kilichopo sasa viongozi waliopo wanatakiwa kuendeleza pale tulipoishia kama kweli wana nia ya kuendesha kklabu hiyo kisasa kwa mtindo wa kampuni.”

Malinzi alisema yeye ni mmoja wa wana hisa kwenye kampuni hiyo ya Yanga, wengine ni Francis Kifukwe, Ibrahim Didi, Abbas Tarimba na David Lwimbo.

Kuelekea mchakato huo kulizuka mgogoro mkubwa na kuigawa Yanga vipande vitatu; Yanga Kampuni iliyokuwa chini ya Kifukwe, Yanga Asili chini ya Yusuph Mzimba na Yanga Academia iliyokuwa chini ya Costantine Merinyo ‘Kibo’.
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 maoni:

Chapisha Maoni

Item Reviewed: Description: Rating: 5 Reviewed By: Unknown
Scroll to Top