Ijumaa, 18 Oktoba 2013

Aliyefungiwa miaka 20 aivimbia TFF

RICHARD Rukambura anatembea na rufaa yake mkononi na ndani ya siku mbili atatinga Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza kupinga adhabu ya kufungiwa kujihusisha na soka kwa miaka 20.

Rukambura amefungiwa kwa muda huo na Kamati ya Maadili ya Rufaa baada ya kupeleka masuala ya soka katika mahakama za kawaida kinyume na Ibara ya 75 ya Katiba ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na kifungu cha 73 (3) (b) cha Kanuni za Maadili za TFF toleo la 2013. Adhabu yake itamalizika Oktoba 15, 2033.

Rukambura amekumbwa na adhabu hiyo baada ya kufungua kesi Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza kupinga kuenguliwa kwenye uchaguzi wa awali wa shirikisho hilo uliokuwa ufanyike Februari 23 mwaka huu.

Hata hivyo, uchaguzi huo ulifutiliwa mbali na shirikisho la kimataifa la mchezo huo, Fifa,  baada ya baadhi ya wagombea kuenguliwa kwenye kinyang’anyiro hicho na kupeleka malalamiko yao huko. Fifa iliingilia kati na kufuta mchakato mzima wa uchaguzi na kuagiza mchakato uanze upya na

Lakini jana Jumatano Rukambura alisema: “Sitakubali kukatwa, kama ‘mbwai na iwe mbwai’ nitahakikisha nakata rufaa mahakamani ndani ya siku mbili hizi, kwa vile ndicho wanachokitaka TFF ili waendelee kubaki madarakani.

“Nimesema sikubali, kamati ya maadili ambayo ilinisafisha ina majaji na mawakili, hiyo kanuni ya kunifungia sikubaliani nayo, nitahakikisha haki yangu naipata mahakamani.

“Katiba ya TFF imesajiliwa na msajili wa vyama vya michezo kwa sheria ya nchi iliyotungwa na Bunge na si kanuni za Fifa, wanapaswa kuheshimu vyombo vya mahakama, mimi nitakwenda mahakamani liwalo na liwe.”

  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 maoni:

Chapisha Maoni

Item Reviewed: Description: Rating: 5 Reviewed By: Unknown
Scroll to Top