Jumapili, 5 Aprili 2015

Katika hali isiyokuwa ya kawaida waumini wa kanisa katoliki mjini Shinyanga wamejikuta wakikaguliwa na jeshi la polisi

 Katika hali isiyokuwa ya kawaida waumini wa kanisa katoliki mjini Shinyanga wamejikuta wakipigwa bumbuazi/kushangaa baada ya kufika katika kanisa la Mama mwenye Huruma la Ngokolo mjini Shinyanga kwa ajili ya ksuhiriki Ibada ya Mkesha wa Pasaka,ambapo kila mmoja alilazimika kukaguliwa kama amebeba silaha na kuingia nayo kanisani.Malunde1 blog imeshuhudia waumini wengi wa kanisa hilo wakiwa wanakaguliwa na askari wa jeshi la polisi usiku wa kuamkia leo huku sababu ikitajwa kuwa ni kuimarisha usalama kwa waumini ili washerehekee sikukuu kwa amani zaidi-Picha zote na Kadama Malunde-Malunde1 blog
 Muonekano wa kanisa Katoliki la Mama mwenye Huruma Ngokolo mjini Shinyanga-
 Waumini wa kanisa katoliki wakiwa nje ya kanisa la Mama Mwenye Huruma wakisubiri kukaguliwa-Kitendo cha kukaguliwa kabla ya kuingia kanisani kinaelezwa kuwa hakijawahi kutokea katika kanisa hilo.
 Askari akimkagua muumini.Hata hivyo akizungumza na Malunde1 blog kwa njia ya simu kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga Justus Kamugisha aliwaondoa hofu wananchi na kudai kuwa zoezi hilo ni la kawaida tu.

"Hizi ni taratibu za kiusalama,wala hakuna haja ya mtu kuhoji,kwani hivi sana kuna watu wanadiriki kuingia na silaha makanisani mfano huko Kisarawe kuna mtu kakamatwa na silaha kanisani,hali ambayo inatishia usalama,kwa hiyo zoezi hili ni la kawaida tu hakuna haja ya kushangaa,tunataka wananchi washerehekee sikukuu kwa amani zaidi",alisema Kamanda Kamugisha

 Zoezi la ukaguzi linaendelea-waumini hao walilazimika kupanga mstari ,na kuanza kukaguliwa mmoja baada ya mwingine na kuruhusiwa kuingia kanisani jambo ambalo liliwashanghaza kwani haijawahi kutokea ikiwa ni mara yao ya kwanza kukaguliwa kama wana silaha.
                         Waumini wakisubiri kukaguliwa katika foleni ya wanawake
                                                                  Kila mmoja alikaguliwa
                                                                                       Nje ya kanisa

Malunde1 blog inalipongeza jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga kwa kuimarisha usalama wa wananchi na mali zao katika sikukuu hii ya Pasaka. Tuwataka wananchi kusherehekea kwa amani sikukuu hii.Lakini pia tunataka pale mnapotoka majumbani muache walau mtu mmoja wa kulinda nyumba kutokana na ukweli uliopo kwamba baadhi ya watu wasiokuwa waaminifu kutumia fursa za sikukuu kufanya uhalifu.

  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 maoni:

Chapisha Maoni

Item Reviewed: Katika hali isiyokuwa ya kawaida waumini wa kanisa katoliki mjini Shinyanga wamejikuta wakikaguliwa na jeshi la polisi Description: Rating: 5 Reviewed By: Unknown
Scroll to Top