Jumatatu, 16 Februari 2015

Netanyahu atakiwa asiende kuhutubia Kongresi

Wazayuni walio wengi wanamtaka Benjamin Netanyahu Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel afute mpango wake wa kutaka kuhutubia Kongresi ya Marekani mwezi ujao. Uchunguzi wa maoni uliofanyika huko Israel unaonyesha kuwa, Wazayuni walio wengi wanaamini kwamba mpango huo wa Netanyahu utasababisha kutokea mpasuko na mivutano zaidi kati ya Tel Aviv na Washington. John Boehner Spika wa Bunge la Marekani amemualika Netanyahu ili akahutubie kwenye baraza hilo mwezi ujao, hotuba ambayo inatarajiwa kujikita zaidi katika masuala ya kuwekwa vikwazo zaidi vya Wamagharibi dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran. Hayo yanajiri katika hali ambayo, Rais Barack Obama amepinga vikali mpango wa kuwekwa vikwazo zaidi dhidi ya Iran na kusisitiza kuwa, kuchukuliwa hatua hiyo kutasababisha kuvurugika mwenendo wa mazungumzo ya nyuklia kati ya Iran na kundi la 5+1. Obama pia amesema kuwa, hana mpango wa kukutana na Netanyahu atakapoizuru Marekani. Uchunguzi huo wa maoni unaonyesha kuwa, asilimia 62 ya Wazayuni wanaamini kwamba, hotuba ya Benjamin Netanyahu haitaweza kuathiri makubaliano yajayo ya nyuklia kati ya Iran na nchi sita zenye nguvu duniani ambazo ni Uingereza, Ufaransa, Russia, China, Marekani na Ujerumani.
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 maoni:

Chapisha Maoni

Item Reviewed: Netanyahu atakiwa asiende kuhutubia Kongresi Description: Rating: 5 Reviewed By: Unknown
Scroll to Top