Jumatatu, 23 Desemba 2013

ZITTO KABWE ASISITIZA HANG'OKI CHADEMA, ASHUTUMU SLAA NA MBOWE KWA UBABAISHAJI

 Sehemu ya wananchi wa mjini Kasulu waliojitokeza kusikiliza hotuba ya zito kabwe ambayo sehemu kubwa ilihusu kupinga kuvuliwa madaraka ndani ya chama chake pamoja na kuwataka wananchi kuungana kuwapinga viongozi wa Kamati kuu ya CHADEMA iliyowavua uongozi Zitto Kabwe, Dr. Kitilya Mkumbo na Migamba kwa tuhuma za Uhaini na usaliti kwa chama hicho
 ZITTO KABWE aliyekuwa Naibu Katibu mkuu na naibu msemaji wa Kambi ya Uoinzani Bungeni (aliyevaa nguo za asili) Muda mfupi baada ya kuvalishwa mavani ya kitemi na wazee wa Heru juu katika JImbo la Kasulu Mjini, kabla ya kuanza kuwahutubia maelfu waliofurika uwanjani hapo. Mkutano huo uliandaliwa na kundi la viongozi wa CHADEMA jimbo ambao pia hivi karibuni wamefukuzwa uongozi na chama hicho ngazi ya wailaya kwa kile kinachotajwa kuwa ni kumuunga mkono ZItto na kupinga uamuzi wa kamati kuu

Viongozi wa Chadema kadhaa hasa wa ngazi za juu wilaya ya Kasulu hawakujitokeza katika mkutano huo.


 Maelfu ya wakazi wa Mji wa Kasulu mkoani Kigoma wakimsikiliza mbunge wa Kigoma Kaskazini (aliyefukuzwa unaibu katibu mkuu wa Chadema) wakati akihutubia mkutano wa hadhara katika uwanja ambapo Dr. Slaa alishambuliwa na wananchi wanaopinga kamati kuu ya chama hicho kumfykuza uongozi ZITTO
 Moja kati ya mabango ya wnanchi ambao walikuwa kwenye mapozi ya mbunge wa jimbo la kigoma  kasikazini Bw. Zitto wakati akiwa wilaya ya kasulu mkoani Kigoma
 Na hayo nikati ya mengi yaliyokuwepo katika mapokezi ya mbunge huyo.

ZITTO AMLIPUA MBOWE -POSHO ZA BUNGE NA MASHANGINGI 

 Mbunge wa Kigoam Kaskazini Zitto Kabwe amelipua kwa wananchi Mwenyekiti wake wa Taifa Freeman Mbowe kwa kukiuka taratibu na kanuni za Bunge kwa kujipatia fedha za kazi za Bunge na kisha kuzitumia kwa anasa

Hayo yametajwa na Zito Kabwe wakati akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara mjini Kasulu akijibu hoja za kamati kuu kumvua madaraka yake ya kichama

Zitto amesisitiza kuwa viongozi wake wa chama wanajaribu kuyumbisha hoja muhimu kama vile, kuchukua fedha za bunge na kwenda kutanua, kukataa mahesabu ya chama kukaguliwa, kuchukua mashangingi na kupokea posho kinyume na makubaliano na kanuni za chama chao.

amesisitiza kuwa kamwe hata kaa kimya na kwamba ataendelea kupinga jambo lolote ambalo linaenda kinyume na maadili ya CHADEMA na hataondoka katika chama hichou licha ya kuwepo kwa shinikizo kubwa

chama chetu tumehangaika kukijenga, sasa wapo wambao waliingia kwa hiyari CHADEMA na wapo ambao walifukuzwa CCM, au walikosa kura za Maoni CCM ndipo wakaja katika chama chetu na hao ndio wanataka wao waonekane wanakijua chama na wana uchungu nacho kuliko sisi tulioingia kwa hiyari na mapenzi yetu kwa demokrasia" alisisitiza Kabwe

Ikumbukwe kuwa Katibu mkuu wa CHADEMA Dr. Wilbroad Slaa kabla ya kujiunga na chama hicho alikuwa mgombea wa CCM na alikimbilia huko baada ya kushindwa katika kura za maoni katika uchaguzi wa ndani ya CCM Jimbo la Karatu

  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 maoni:

Chapisha Maoni

Item Reviewed: Description: Rating: 5 Reviewed By: Unknown
Scroll to Top