Jumatatu, 23 Desemba 2013

WABUNGE WA UPINZANI WATAJWA KUULIZA MASWALI NA HOJA ZA KUTUMWA BUNGENI

Imebainika kuwa baadhi ya wabunge wa majimbo hawna uwezo wa kujenga hoja wala kusimamia jambo lolote bungeni, wawapo katika vikao inapoibuka hoja yoyote hutegemea wabunge wenzao kuwaandalia maswali au kuwashinikiza kuuliza maswali hasa yanayolenga kuihujumu serikali.

Hayo yemebainika pia katika kikao cha Bunge siku ya ijumaa December 20 wakati wa kujadili taarifa ya kamati ya kudumu ya ardhi maliasili na mazingira iliyokuwa ikijadili kuhusu ukiukwaji wa miongozo wakati wa operesheni Tokomeza, Baadhi ya wabunge wakiwemo wa mkoa wa Kigoma waliuliza maswali ya kutumwa au kutungwa na wenzao na wao kuwa vipaza sauti tu.

Je kwa karne hii ya sayansi na teknolojia Bado Tanzania inahitaji wabunge ambao wao hawana la kuliambia taifa hadi washawishiwe au wahinikizwe na wabunge wenzao? Je Upinzani tunaopigania kuujenga ili kupambana na CCM unajengwa kwa njia ya mashinikizoo na maswali ya kuongozwa na wengine
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 maoni:

Chapisha Maoni

Item Reviewed: Description: Rating: 5 Reviewed By: Unknown
Scroll to Top