Jumatano, 23 Oktoba 2013

HAMISI KIIZA 'DIEGO WA JANGWANI' BADO BAO MOJA TU KUMKAMATA TAMBWE SIMBA SC




HAMISI Friday Kiiza ‘Diego’ wa Yanga SC leo hii amefikisha mabao saba katika mbio za ufungaji bora wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, baada ya kufunga mabao mawili katika ushindi wa 3-0 dhidi ya Rhino


Rangers Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Hii inakuwa mechi ya pili mfululizo Mganda huyo anafunga mabao mawili kila mechi, baada ya Jumapili pia kufunga mara mbili katika sare ya 3-3 na wapinzani wa jadi, Simba SC Uwanja huo huo wa Taifa, Dar es Salaam.


Kiiza sasa anazidiwa kwa bao moja tu mchezaji anayeongoza mbio hizo, Mrundi, Amisi Tambwe wa Simba SC, ambaye mechi tatu sasa hajafunga bao.  
 
Mshambuliaji huyo wa timu ya taifa ya Uganda, The Cranes analingana na mshambuliaji chipukizi wa kimataifa wa Tanzania, Juma Luizio wa Mtibwa Sugar ambaye pia ana mabao saba.
 
Wanaofuatia ni Elias Maguri wa Ruvu Shooting mwenye mabao sita, Themi Felix wa Kagera Sugar mwenye mabao matano sawa na Tumba Swedi wa Ashanti, wakati Didier 

Kavumbangu wa Yanga SC ana ambao manne sawa na Kipre Tchetche Azam FC ambaye ndiye anashikilia tuzo ya ufungaji bora wa ligi hiyo


WANAOONGOZA KWA MABAO LIGI KUU:

JINA                    TIMU   MABAO

Amisi Tambwe     Simba SC    8
Hamisi Kiiza        Yanga SC    7
Juma Luizio         Mtibwa        7
Elias Maguri        Ruvu Shoot 6
Themi Felix          Kagera       5
Tumba Swedi      Ashanti       5
D. Kavumbangu  Yanga SC   4
Kipre Tchetche    Azam FC    4

  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 maoni:

Chapisha Maoni

Item Reviewed: Description: Rating: 5 Reviewed By: Unknown
Scroll to Top