Jumatano, 23 Oktoba 2013



             HABARI KUTOKA STANDARD RADI SINGIDA TANZANI                

* Watu wanne wamehukumiwa kifungo cha miaka 30 Jela kwa kosa la unyang’anyi wa zaidi ya shilling milioni nane kwa kutumia silaha



* Vyama vya siasa vilivyo na uwakilishi, kikiwamo Chama Cha Mapinduzi (CCM) na visivyokuwa na uwakilishi bungeni vimewasilisha mapendekezo ya kuboresha marekebisho ya Sheri ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2013.


* Shirika la mpango wa chakula duniania WFP amesema kuna uwezekano wa kupunguzwa misaada ya chakula inayopelekwa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kutokana na kupungua fedha za taasisi hiyo.


* Jeshi la Nigeria limewaua wanamgambo 37 wanaodhaniwa kuwa wanachama wa kundi la Boko Haram huko kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.  

HABARI KAMILI

Source; Sr/Raymond/Operation
Ed;
Date; 23/10/2013

SINGIDA
Mkoa wa singida unatarajia kuanza operation ya ukaguzi wa kubaini watu wanaoishi nchini kinyume na sheria.


Hayo yamebainishwa jana na Afisa uhamiaji mkoa wa Singida Bw. Adam Mnyeke wakati akizungumza katika siku maalum ya polisi iliyofanyika katika ukumbi wa Aquar Manispaa ya Singida,


Bw. Mnyeke amesema kuwa zoezi hilo linatarajia kuanza wiki ijayo, hivyo kutoa wito kwa wananchi kuotoa ushirikiano kwa taasisi hiyo ili kupambana na wahamiaji haramu.


Amesema kwa kuanza, zoezi hilo litaanzia manispaa ya singida na baadaye litakwenda katika wilaya nyingine za mkoa wa Singida, na kuongeza kuwa zoezi hilo pia litasaidia kupambana na vitendo vya uhalifu ambavyo mara nyingi vimekuwa vikifanywa na wahamiaji haramu.

Source; Sr/Chami/Mahakamani
Ed;
Date; 23/10/2013

SINGIDA
Watu wanne wamehukumiwa kifungo cha miaka 30 Jela kwa kosa la unyang’anyi wa zaidi ya shilling milioni nane kwa kutumia silaha


Akisoma hukumu hiyo hakimu mfawidhi wa mahakama ya wilaya mkoani Singida Flora Ndale amesema tukio hilo limetokea desember 8 waka 2012 katika barabara ya singida kwenda Dodoma maeno ya kisaki


Amesema siku ya tukio washtakiwa waliweka mawe barabarani na kuteka gari lililokua likisafirisha maiti ya mwanafuzi wa chuo kikuu cha Sokoine {SUA] kutoka morogoro kuelekea Tarime


Katika tukio hilo vitu mbalimbali kama laptop, simu za mkononi, moderm mbili zote vikiwa na thamani ya shilingi milioni nane laki saba viliibwa


Amewataja waliohukumiwa kuwa ni Hamisi Issa, Halidi Hamisi, Abbubakari Jumanne, Hamisi Alli wote wakazi wa mkoa wa Singida,ambapo siku ya tukio walikuwa na rungu,mawe na mashoka wakitumia kufanya uhalifu huo


Hakimu Ndale amesema kitendo hicho ni amesema adhabu hiyo itakua fundisho kwa watu wengine wanaofanya vitendo kama hivyo.









Source; Sr/Raymond/uhalifu
Ed;
Date; 23/10/2013

SINGIDA
Mkoa wa Singida ni miongoni mwa mikoa minne nchini iliyofanikiwa kupambana na vitendo vya uhalifu kwa kiwango kikubwa kwa kipindi cha hivi karibuni.


Mratibu  wa Polisi kutoka makao makuu Dar es salaam kitengo cha maadili James Kasusura amesema hayo wakati akizungumza na washiriki wa kikao cha siku maalum ya polisi kilichofanyika katika ukumbi wa Aquar manispaa ya Singida.


Kasusura ameyataja makosa yaliyopungua kuwa ni makosa dhidi ya ubinadamu ambayo yamepungua kwa asilimia 35, makosa dhidi ya mali yamepungua kwa asilimia 18, makosa dhidi ya maadili yamepungua kwa sailimia 13, na makosa dhidi ya usalama barabarani yamepungua kwa asilimia 12.


Amesema kupungua kwa makosa hayo kumetokana na ushirikiano baina ya raia na vyombo vya ulinzi na usalama mkoani Singida, hivyo kutoa wito wa kuendelezwa kwa ushirikiano huo na hatimae kukomesha vitendo hivyo kabisa.


Source; Sr/Raymond/uhalifu
Ed;
Date; 23/10/2013

DAR ES SALAAM
Vyama vya siasa vilivyo na uwakilishi, kikiwamo Chama Cha Mapinduzi (CCM) na visivyokuwa na uwakilishi bungeni vimewasilisha mapendekezo ya kuboresha marekebisho ya Sheri ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2013.


Msemaji wa vyama hivyo, ambaye pia ni mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, Bw James Mbatia, amesema kuwa mapendekezo hayo yalikabidhiwa kwa waziri wa Nchi, Ofisi ya waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi.


Miongoni mwa waliohudhuria kikao hicho ni pamoja na katibu mkuu wa Chadema, Dk. Willibrod Slaa, makamu mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Philip Mangula, na mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba.


Mbatia amesema  kwamba wamekubaliana  mapendekezo hayo yapelekwe katika mkutano ujao wa Bunge unaotarajiwa kuanza wiki ijayo kwa hati ya dharura.


UNAENDELEA KUSOMA TAARIFA YA HABARI KUTOKA STANDARD RADIO NA SASA NI HABARI ZA KIMATAIFA.
 
Source: BBC Im( usalaama)
Ed
Date: Wednesday  October 23, 2013
KINSHASA
Shirika la mpango wa chakula duniania WFP amesema kuna uwezekano wa kupunguzwa misaada ya chakula inayopelekwa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kutokana na kupungua fedha za taasisi hiyo.

Msemaji wa taasisi hiyo amesisitiza kuwa, shirika hilo limepokea asilimia 50 tu ya fedha inazohitajia kwa ajili ya kusaidia chakula katika kipindi cha miezi 6 ijayo.

Aidha amesema mpango wa Chakula Duniani unakabiliwa na upungufu wa dola milioni 70  hivyo unalazimika kupunguza misaada kuanzia mwezi november

Upungufu huo wa misaada ya chakula utawaathiri karibu wakimbizi laki 3 wanaohitajia misaada ya chakula katika mkoa wa Kivu Kaskazini, mashariki mwa Kongo. Asilimia 60 ya familia za mkoa huo zinakabiliwa na uhaba wa chakula

Source: BBC Im( usalaama)
Ed
Date: Wednesday  October 23, 2013
JUBA
Raia 856 wa Sudan Kusini waliokuwa wakiishi Sudan wamewasili mjini Juba baada ya kusafiri  kwa siku 17  kwa kutumia jahazi

Kwa miaka kadhaa sasa mpango wa wananchi hao kurejea Sudan Kusini ulikuwa unakwama kwenye mpaka wa kaskazini  katika eneo la Renk

Msemaji wa shirika la IOM  Bw Jumbe Omari Jumbe amesema kupitia mpango wa usaidizi wa kurejea nyumbani uitwao OTA, IOM kuanzia mwaka huu  imesaidia watu elfu sita wa  sudan kusini kurejea kwao

Amesema zoezi la utambuzi lililofanyika katikati ya mwaka huu huko Renk lilibaini kuwepo kwa watu Elfu Tatu waliokwama eneo hilo wakisubiri kuelekea Sudan Kusini.

Source: BBC  Im (vifo)
Ed
Date: Wednesday  October 23, 2013
ABUJA


Jeshi la Nigeria limewaua wanamgambo 37 wanaodhaniwa kuwa wanachama wa kundi la Boko Haram huko kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.

Msemaji wa jeshi la Nigeria katika jimbo la Borno kaskazini mashariki mwa nchi hiyo Kapteni Aliyu Danja amesema jeshi lilifanya mashambulizi dhidi ya kambi ya Boko Haram huko Alagano.

Kapteni Danja ameongeza kuwa oparesheni hiyo iliyoanza juzi Jumatatu ilihusisha mashambulizi ya nchi kavu na angani kwa lengo la kuisambaratisha ngome ya wanamgambo wa Boko Haram huko Alagano. 

Mwezi Mei 15 mwaka huu jeshi la Nigeria lilianzisha mashambulizi dhidi ya kundi la Boko Haram siku moja baada ya Rais Goodluck Jonathan kutangaza hali ya hatari kwenye majimbo matatu ya Borno, Yobe na Adamawa kaskazini mashariki mwa nchi hiyo

Kabla ya kumaliza kusoma  taarifa ya habari huu tena ni muhtasari wake

* Watu wanne wamehukumiwa kifungo cha miaka 30 Jela kwa kosa la unyanganyi wa zaidi ya shilling milioni nane kwa kutumia silaha



* Vyama vya siasa vilivyo na uwakilishi, kikiwamo Chama Cha Mapinduzi (CCM) na visivyokuwa na uwakilishi bungeni vimewasilisha mapendekezo ya kuboresha marekebisho ya Sheri ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2013.


* Shirika la mpango wa chakula duniania WFP amesema kuna uwezekano wa kupunguzwa misaada ya chakula inayopelekwa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kutokana na kupungua fedha za taasisi hiyo.


* Na Jeshi la Nigeria limewaua wanamgambo 37 wanaodhaniwa kuwa wanachama wa kundi la Boko Haram huko kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.  

Na huo ndio mwisho wa taarifa ya habari kutoka standard redio 
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 maoni:

Chapisha Maoni

Item Reviewed: Description: Rating: 5 Reviewed By: Unknown
Scroll to Top